Jumapili, 25 Desemba 2016

Guardiola:messi ni zaidi ya ronaldo

Guardiola amesema yake juu ya mdahalo unaovuma kuhusu mchezaji bora wa dunia baada ya Cristiano Ronaldo kutwaa tuzo ya nne ya Ballon d’Or mwezi huu
Meneja huyo wa Manchester City ambaye anaiandaa timu yake kwa mechi ya Ligi Kuu Uingereza dhidi ya Hull City Jumatatu, alikuwa na miaka minne ya mafanikio kama bosi wa Barcelona na alimfundisha Lionel Messi – ambaye ni mpinzani mkubwa wa Mreno huyo katika tuzo, na pia bado anaamini Messi ni zaidi ya Ronaldo.
Baada ya kocha wa sasa wa Nou Camp,
Luis Enrique kusisitiza kuwa Messi bado ni mchezaji bora wa dunia huku akiponda maamuzi ya Ballon d’Or kwenda kwa CR7, Mhispania mwenzake naye amemuunga mkono.
Akizungumza katika mkutano wa mahojiano na waandishi kuhusu mechi ya Hull City dhidi ya Man City, hiki ndicho alichosema Guardiola: “Nakubaliana na Luis Enrique. Messi ni bora, nab ado ataendelea kuwa. Naam ni bora zaidi.
“Kwa sababu anajua namna ya kucheza, namna ya kufunga magoli. Kwa sababu ndivyo alivyo… kwa heshima zote kwa wachezaji wote ambao wameshinda, na shukrani kwa Cristiano, lakini bado Leo yupo juu zaidi.
Privacy Policy Terms of Service About Us
Contact Us
Copyright © 2016 Goal.com All rights reserved. The information contained in Goal.com may not be published, broadcast, rewritten, or redistributed without the prior written authority of Goal.com
12/24/16 LA LIGA
Getty Images

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni