Mchezaji Yaya Toure amesema hawezi kutafuta klabu ya kuhamia katika kipindi hichi cha mwezi Januari na badala yake anaangalia zaidi kusaidia klabu yake ya Manchester City.
Toure mwenye umri wa miaka 33, amebakisha miezi sita ya mwisho ya mkataba wake Etihad na yuko huru kuanza kuwasiliana na klabu nyingine.
Lakini amesema: “Kwa sasa naangazia City. Siku za usoni zipo lakini kwa sasa ligi bado haijamalizika.”
Raia huyo wa Ivory Coast alirejeshwa kucheza Novemba baada ya kuwekwa kwenye benchi kwa miezi mitatu kutokana na matamshi ya wakala wake.
Kocha wa City Pep Guardiola alikuwa ameapa kutomchezesha Toure hadi wakala wake Dimitri Seluk aombe msamaha kwa kusema Toure aliaibishwa kwa kutojumuishwa kikosi cha City kinachocheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Toure aliomba msamaha kwa niaba ya Seluk mwezi Novemba na amekuwa kiungo muhimu katika timu yake.
Alipo rejea katika mechi yake ya kwanza aliifungia timu yake mabao mawili ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Crystal Palace tarehe 19 Nove
Jumatano, 4 Januari 2017
Yaya toure sina mpango wa kuondoka city
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni