Jumatatu, 2 Januari 2017

Azam yashinda moja,kombe la mapinduzi

BAO pekee la mshambuliaji chipukizi, Shaaban Iddi Chilunda limetosha kuipa Azam FC ya Dar es Salaam ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Zimamoto katika mchezo wa Kundi B Kombe la Mapinduzi.
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar jioni ya leo, Chilunda alifunga bao hilo dakika ya 79 akimvisha kanzu kipa baada ya kuipokea kiufundi kwa kifua pasi ya juu ya kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Mchezo wa pili wa kundi hilo unafuatia Saa 2:30 usiku wa leo kati ya Yanga SC ya Dar es Salaam na Jamhuri ya Pemba, Uwanja wa Amaan pia, hapa Zanzibar.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni