Je! Usajili wa Ndidi kutoka Genk una madhara yoyote kwa maisha ya soka ya Mbwana Samatta anayekipiga katika klabu hiyo ya Ubelgiji?
Leicester City hatimaye wametangaza rasmi usajili wa Wilfred Ndidi kutoka Genk
kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 15 baada ya kibali cha kufanya kazi Uingereza kuidhinishwa.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria alifaulu vipimo vya afya kujiunga na Leicester mapema wiki hii na alikubari vigezo na masharti kusaini mkataba wa miaka mitano.
Je! Usajili wa Ndidi kutoka Genk una madhara yoyote kwa maisha ya soka ya
Mbwana Samatta anayekipiga katika klabu hiyo ya Ubelgiji?
Ni wazi kama Samatta alifikiria kuuzwa dirisha la uhamisho wa Januari uwezekano wa yeye kuondoka Genk ni mdogo, kwani klabu haiwezi kukubali kupoteza mchezaji mwingine zaidi mwenye uwezo.
Kwa upande mwingine kutupiwa virago kwa kocha aliyemsajili Samatta kunaweza kuwa moja ya mambo yanayomsukuma Samatta kutamani kuondoka Genk kwani hana uhakika kama ataweza kumshawishi kocha mpya, lakini wazo la kuondoka halitakuwa rahisi kutimia kufuatia kuondoka kwa Ndidi aliyetua Leicester.
Ndidi, ambaye uchezaji wake umefananishwa na ule wa nyota wa zamani wa Leicester N’Golo Kante yupo tayari kucheza mechi za wikiendi za Kombe la FA dhidi ya Everton baada ya kufanya mazoezi na wachezaji wenzake wa klabu yake mpya kwa mara ya kwanza Alhamisi.
“Kila kitu kuhusu kibali cha kazi kipo sawa,” meneja Claudio Ranieri aliwaambia waandishi. “Amefanya mazoezi leo. Yupo tayari kwa mechi ya Jumamosi, na mambo yote yako poa. Sina uhakika [kama atacheza]. Ngoja niendelee kumchunguza katika mazoezi. Leo ilikuwa mara yake ya kwanza. Nadhani kesho nitamwangalia zaidi na kisha nitaamua.
“Ni mchezaji mwenye mvuto na mwenye mustakabali angavu. Ni mrefu na anaruka vizuri sana kwa ajili ya mipira ya kichwa, hukimbiza mpira haraka na mwepesi kutafuta mpira.
“Tumemfuatilia sana na tunatumai kwa haraka atawavutia mashabiki. Ni mchezaji mwingine tofauti na [Kante] – tofauti kabisa. Timu nyingi kubwa zilimtaka, lakini akapendelea kujiunga nasi ili aimarike zaidi.”
Jamie Vardy pia anatarajiwa kucheza mechi hiyo ya Kombe la FA katika uwanja wa Goodison Park baada ya kumaliza adhabu yake ya kufungiwa mechi tatu, wakati Islam Slimani akiwa bado hajapona vizuri kupangwa kwenye kikosi.
Privacy Policy Terms of Service About Us
Contact Us
Copyright © 2017 Goal.com All rights reserved. The information contained in Goal.com may not be published, broadcast, rewritten, or redistributed without the prior written authority of Goal.com
22:04 TANZANIANS ABROAD
Getty
NEXT ARTICLE
Ijumaa, 6 Januari 2017
Ndidi atimkia leicester je samatha?
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni