Je! Usajili wa Ndidi kutoka Genk una madhara yoyote kwa maisha ya soka ya Mbwana Samatta anayekipiga katika klabu hiyo ya Ubelgiji?
Leicester City hatimaye wametangaza rasmi usajili wa Wilfred Ndidi kutoka Genk
kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 15 baada ya kibali cha kufanya kazi Uingereza kuidhinishwa.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria alifaulu vipimo vya afya kujiunga na Leicester mapema wiki hii na alikubari vigezo na masharti kusaini mkataba wa miaka mitano.
Je! Usajili wa Ndidi kutoka Genk una madhara yoyote kwa maisha ya soka ya
Mbwana Samatta anayekipiga katika klabu hiyo ya Ubelgiji?
Ni wazi kama Samatta alifikiria kuuzwa dirisha la uhamisho wa Januari uwezekano wa yeye kuondoka Genk ni mdogo, kwani klabu haiwezi kukubali kupoteza mchezaji mwingine zaidi mwenye uwezo.
Kwa upande mwingine kutupiwa virago kwa kocha aliyemsajili Samatta kunaweza kuwa moja ya mambo yanayomsukuma Samatta kutamani kuondoka Genk kwani hana uhakika kama ataweza kumshawishi kocha mpya, lakini wazo la kuondoka halitakuwa rahisi kutimia kufuatia kuondoka kwa Ndidi aliyetua Leicester.
Ndidi, ambaye uchezaji wake umefananishwa na ule wa nyota wa zamani wa Leicester N’Golo Kante yupo tayari kucheza mechi za wikiendi za Kombe la FA dhidi ya Everton baada ya kufanya mazoezi na wachezaji wenzake wa klabu yake mpya kwa mara ya kwanza Alhamisi.
“Kila kitu kuhusu kibali cha kazi kipo sawa,” meneja Claudio Ranieri aliwaambia waandishi. “Amefanya mazoezi leo. Yupo tayari kwa mechi ya Jumamosi, na mambo yote yako poa. Sina uhakika [kama atacheza]. Ngoja niendelee kumchunguza katika mazoezi. Leo ilikuwa mara yake ya kwanza. Nadhani kesho nitamwangalia zaidi na kisha nitaamua.
“Ni mchezaji mwenye mvuto na mwenye mustakabali angavu. Ni mrefu na anaruka vizuri sana kwa ajili ya mipira ya kichwa, hukimbiza mpira haraka na mwepesi kutafuta mpira.
“Tumemfuatilia sana na tunatumai kwa haraka atawavutia mashabiki. Ni mchezaji mwingine tofauti na [Kante] – tofauti kabisa. Timu nyingi kubwa zilimtaka, lakini akapendelea kujiunga nasi ili aimarike zaidi.”
Jamie Vardy pia anatarajiwa kucheza mechi hiyo ya Kombe la FA katika uwanja wa Goodison Park baada ya kumaliza adhabu yake ya kufungiwa mechi tatu, wakati Islam Slimani akiwa bado hajapona vizuri kupangwa kwenye kikosi.
Privacy Policy Terms of Service About Us
Contact Us
Copyright © 2017 Goal.com All rights reserved. The information contained in Goal.com may not be published, broadcast, rewritten, or redistributed without the prior written authority of Goal.com
22:04 TANZANIANS ABROAD
Getty
NEXT ARTICLE
HABARIHOTZ
Ijumaa, 6 Januari 2017
Ndidi atimkia leicester je samatha?
Jcb awaponda mashabiki wake baada ya kumkejeri kwanini katemblea ofisi za WCB
Rapper JCB amewashangaa baadhi ya mashabiki wa hip hop waliomkejeli baada ya kuzitembelea ofisi za WCB hivi karibuni. Akiwa kwenye ofisi hizo, JCB alipiga picha na Ray Vann na Babutale.
“Dah wapenda #HipHop ni watu wa ajabu sana eti kupiga picha na baadhi ya wasanii kutembelea studio flani kwao ni kosa,” ameandika kwenye akaunti yake ya Facebook.
“Wakati huo huo hao wanaojiita #Wanaharakati wa #HipHop hana mchango wowote wa kumsaidia huyo msanii wao wanao mwita mwana Hip hop kama kuja kwenye show kununua cd kununua tshet.”
“Wana subiri tudate au tuvute unga ndo watuongelee tena kwa mabaya….wacheni hizo nyie hizi ni picha tu mnachanganyikiwa na kutukana sasa hilo lingoma likishuka itakuaje.”
Mbuyu twite atua omani
Baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Yanga mchezaji Mbuyu Twite ambaye anaweza kucheza kama kiungo amejiunga na
timu ya Fanja ya Oman.
Twite amesha anza mazoezi na timu yake hiyo ya mjini Muscat Oman, Twite aliutumikia klabu ya Yanga kwa miaka minne, mchezaji mwingine ambaye ni Mtanzania anayeichezea Fanja ni mshambuliaji Danny Lyanga wa Simba ambaye yuko kwa mkopo katika timu hiyo.
Ujumbe wa mehrez baada ya kushnda tuzo
Ni furaha kwa kila mtu pindi mchango wake unapoonekana na kupewa zawadi – ndicho kilichomtokea Riyad Mahrez usiku wa Alhamisi hii baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa kuwabwaga washiriki wengine akiwemo Pierre-Emerick Aubameyang na Sadio Mane.
Mahrez ambaye ni mchezaji wa Algeria amewashukuru mashabiki wote duniani kutokana na kuwa na msimu mzuri kwa mwaka jana na kufanikiwa kuisaidia timu yake ya Leicester City kushinda taji la ligi kuu ya Uingereza.
Kupiti kwenye mitandao yake ya kijamii, mchezaji huyo ameandika, “African ballon d’or … I thank everyone who supporte me around Africa and around the world .”
Hii ni tuzo ya tatu kubwa kushinda kwa mchezaji huyu baada ya ile ya ‘Mchezaji bora wa mwaka ya chama cha wachezaji soka ya kulipwa Uingereza (PFA) na ‘BBC African Player of the Year’.
Dyna nyange kuwania tuzo ya bae uko nigeria
Msanii wa Bongo Fleva, Dayna Nyange amechaguliwa kuwania tuzo za BAE Awards 2017 za nchini Nigeria akiwa ni msanii pekee kutoka Tanzania.
Hitmaker huyo wa Komela amechaguliwa katika vipengele viwili ikiwemo kimoja cha BEST AFRICAN ACT akichuana na Eddy Kenzo (Uganda), King Kaka (Kenya), Stoneboy (Ghana), Jah Vinci (Jamaica).
Kipengele kingine anachowania ni BEST VOCAL PERFORMANCE FEMALE kupitia wimbo wake ‘Angejua’ ambapo anawania tuzo hiyo na Aramide, Ngowari na Rocknana (wote kutoka Nigeria)
Kipa denis onyango wa mamelod ashinda tuzo hii
Mchezaji wa klabu ya Memelodi Sundowns ambaye ni golikipa Denis Onyango, raia wa Uganda na ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, msimu uliopita wa mwaka 2015 tuzo hiyo alishinda Mtanzania Mbwana Samata.
Mchezaji bora kwa kina dada imeenda kwa Asisat Oshoala wa Liverpool na timu ya taifa ya Nigeria huku timu bora ya mwaka ikiwa ni Uganda.
A
Aunt ezekiel katuachia funzo juu ya mapenzi
Moja kati ya matatizo ya watanzania, ni kushindwa kusimamia yale tunayoayaamini. Linapokuja suala la mapenzi wengi hujikuta kwenye wakati mgumu hasa ikiwa yule anayempenda anaonekana si wa maana mbele za watu kwa hadhi,kipato na muonekano.
Pengine mwaka 2016 mwanadada Aunty Ezekiel alituachia funzo,ukipenda usiangalie wengine wanaonaje fuata moyo wako na wasipooelewa wengine wataelewa mwisho wa safari.
Miaka michache nyuma ilisemekana mmoja kati ya warembo A-list wa bongo movie Aunty Ezekiel amebeba mimba ya dansa wa kutegemewa wa Diamond Platinumz, Mose Iyobo, haikuaminika na wengi wetu. Sio kwa kuwa Iyobo hatakiwi kupendwa, lahasha ila kwa kuWa imezoeleka mastaa hasa wa bongo movie kudate na watu wenye kipato kikubwa pengine na umaarufu mkubwa. Wengi waliamini Iyobo ni kama amewekwa kupoteza maboya ili watu wasimjue muhusika haswa wa mimba ya Aunty!
Miaka imepita Mose na Aunty wana mtoto wa kike anaitwa Cookie! Unajua nini? Ukipitia kwenye mitandao ya kijamii moja kati ya couple ambaye sasa zinazopostiwa sana ni Mose na Aunty,watu wanawatamani,watu wanaona wanapendezana.
Ingekua Aunty amewasikiliza pengine kusingekuwa na uhusiano. Ingekuwa amemuona kwa jicho wanalomuona wengine pengine penzi lingekufa siku nyingi. Lakini kwa kuwa alimua kuufuata moyo wake na kuamini kuwa yule ambaye wengine wanamuona sio sahihi kwake ndiye haswaa anastahili kukabidhiwa mtima wake,ndio sababu wapo walipo.
Kwa yoyote anayehusika, mapenzi ni baina ya nafsi mbili zinazopendana,ni vema kusikiliza ushauri na kuufanyia kazi lakini maaumizi yabaki ya kwako. Mwisho wa siku wewe ndo unajua sababu ya kumpenda uliyenaye. Haijalishi wanasemaje au wanaonaje juu ya uhusiano wako Shika uliposhikilia kama kuelewa,wataelewa mbele wa safari.
I